Marehemu SACP Aneth Laurent  enzi za uhai wake

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja anasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza - SACP Aneth Laurent kilichotokea jana Julai 30, 2015 katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza.
Kamishna Jenerali wa Magereza anatoa pole kwa Watumishi wote wa Jeshi la Magereza nchini, familia na wale wote walioguswa na msiba huu kwa namna tofauti tofauti.
Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na familia ya Marehemu linaendelea kuratibu shughuli za msiba ambapo mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwa ndege kutoka Mwanza kuja Jijini Dar es Salaam na taarifa za mazishi zitatolewa baadaye baada ya taratibu zote kukamilika.
                    Mwenyezi Mungu ailaze roho ya 
Marehemu mahali pema peponi Amina.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...