THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.

  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com






miondoko ya kumeremeta kwenye mnuso


ngoma azipendazo ankal

Ngoma ya Oliver Ngoma (RiP) 'ADIA' ni balaa


DIAMOND AAHIDI KUMFUNIKA VIBAYA PREZZO SHOO YA USIKU WA MATUMAINI 2013

Diamond akilonga na Sauda kuhusu shoo kali atakayotoa Usiku wa Matumaini 2013.


Na Wilbert Molandi

MKALI wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’ ametamba kufanya shoo kali ikiwemo kumfunika msanii wa Uganda, Prezzo katika Tamasha la Matumaini 2013 litakalofanyika Sikukuu ya Sabasaba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Diamond ametoa majigambo hayo wakati wa mahojiano na Mtangazaji wa kituo cha Star TV, Sauda Mwilima.

“Nimeahidi kufanya bonge la shoo kwenye Tamasha la Matumaini siku hiyo, mashabiki wangu na wapenzi wa muziki wajitokeze kwa wingi.
“Ninataka kudhihirisha ubora wangu siku hiyo kwa kumfunika vibaya Prezzo,” alisema Diamond.


NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ATEMBELEA MAHAKAMA ZA MWANZO ZA WILAYA YA CHAMWINO

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Angella Kairuki (mwenye koti la pink) akimsikiliza Bw. Paschal Mayumba Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Mvumi Makulu anayehudumia Mahakama ya Mwanzo Mvumi Makulu na Mahakama ya Mwanzo ya Handali akitoa ufafanuzi wa jambo kuhusu kiwanja ambacho Mahakama ya Mwanzo ya Handali imepewa na Uongozi wa Kijiji kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Mahakama hiyo. Kushoto kwa Mhe. Kairuki ni Mhe. Livingstone Lusinde, Mbunge wa Jimbo la Mtera, ambaye aliambatana na Naibu Waziri katika kutembelea Mahakama za Mwanzo za Wilaya ya Chamwino. Wengine katika picha hiyo ni viongozi wa Mahakama na viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Handali.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Angella Kairuki akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Makang’wa Wilayani Chamwino na kuwahamasisha kujenga majengo ya Mahakama kwa nguvu zao ili waweze kupata huduma hii muhimu karibu na maeneo yao na kuacha kutembea umbali mrefu kuzifuata mahakama ili kupata haki zao. Aidha,Mhesjhimiwa Kairuki aliwaahidi wananchi hao kwamba Serikali kupitia Mahakama itashirikiana nao katika kujenga jengo la Mahakama katika eneo hilo.
Mbunge wa Jimbo la Mtera, Mhe. Livingstone Lusinde akiuelezea ujumbe wa Mhe. Angellah Kairuki namna ambavyo uongozi wa Mahakama umepewa kiwanja na uongozi wa Kata ya Mvumi Mission kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya la Mahakama ya Mwanzo. Hadi sasa eneo hilo lenye wakazi wengi halina huduma ya Mahakama na hivyo kuwalazimu wananchi wa eneo hilo kutembea umbali mrefu kutafuta haki zao.


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SIKU 4 WA MAWAKALA WA USAFIRISHAJI WA MAJINI KWA NCHI ZA MASHARIKI YA KATI KWA AFRIKA JIJINI DAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, wakati alipowasili kwenye Hoteli ya Double Tree, kwa ajili ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mawakala wa Usafirishaji wa Majini kwa nchi za Mashariki ya Kati kwa Afrika, uliaoanza jijini Dar es Salaam leo Juni 19, 2013 unaofanyika kwa siku nne.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mawakala wa Usafirishaji wa Majini kwa nchi za Mashariki ya Kati kwa Afrika, uliaoanza jijini Dar es Salaam leo Juni 19, 2013 unaofanyika kwa siku nne. 
Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, akizungumza kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, kufungua mkutano huo.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi rasmi wa mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe,wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mkutano huo.Picha na OMR


Siku ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani yaadhimishwa jijini Dar es Salaam leo

Mwenyekiti wa Mfuko wa Sikoseli Tanzania, Grace Rubambey (katikati) akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya ugonjwa wa Sikoseli Duniani jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Mfuko huo, Dk Julie Makani, Balozi wa Canada nchini, Alexandre Leveque na mmoja wa watu wanoishi na ugonjwa huo, Arafa Salim Said.
Balozi wa Canada nchini, Alexandre Leveque (katikati) akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya ugonjwa wa Sikoseli Duniani jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Mfuko wa Sikoseli Tanzania Dk Julie Makani na Mwenyekiti wa mfuko huo, Grace Rubambey na mmoja wa watu wanoishi na ugonjwa huo, Arafa Salim Said.
Makamu Mwenyekiti wa Mfuko wa Sikoseli Tanzania, Dk Julie Makani (kushoto) akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya ugonjwa wa Sikoseli Duniani jijini Dar es Salaam leo. Tanzania ni nchi ya nne duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaougua ugonjwa wa sikoseli.
Meneja wa Benki ya KCB Tawi la Msimbazi, Philipo Pilla (kulia) akizungumza wakati wa maadhjimisho hayo. Benki ya KCB ni mmoja wa wadhamini wa Mfuko wa Sikoseli Tanzania.
Mratibu wa Huduma za Ugonjwa wa sikoseli katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Deogratias Soka (kulia) akizungumza kuhusu hali ya ugonjwa huo katika hospitali hiyo katika maadhimisho hayo. Inakadiriwa kuwa katika ya watoto 8,000 hadi 10,000 kuzaliwa na ugonjwa huo nchini Tanzania kila mwaka.


TANAPA YAKABIDHI MADAWATI 414 KWA MKOA WA MOROGORO

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Allan Kijazi, (mwenye kipaaza sauti ) akitoa maelezo mafupi juu ya mpango endelevu wa kuaidia madawati kwa shule za Msingi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Joel Bendera (akiyeinamisha kichwa na kushika mikono mbele ,Juni 14, mwaka huu kwenye viwanja vya Hoteli ya Twiga ya Hifadhi ya Milima ya Udzungwa , Tanapa ilikabidhi madawati 414 yaliyogharimu sh: milioni 28.9 kwa shule za msingi 17 za Tarafa ya Mang’ula na Kidatu , wilayani Kilombero ukiwa ni mpango endelevu wa kudumisha ujirani mwema na vijiji vinavyopakana na Hifadhi za Taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( kulia) akimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa. Allan Kijazi.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Mang'ula wakimba kwaya wakati wa halfa ya kukabidhiwa madawati na TANAPA.
Baadhi ya watendaji wa Kata za Tarafa ya Mang'ula na Kidatu,wilayani Kilombero.Picha na John Nditi,Globu ya Jamii-Kilombero.


MWENYEKITI WA CHADEMA PAMOJA NA MBUNGE WA ARUSHA MJINI WASAKWA NA JESHI LA POLISI

Na Ripota Wetu,Arusha

Jeshi la Polisi nchini linawasaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Mkuu wa kambi ya upinzani bungeni,Mh. Freeman Mbowe pamoja na Mbunge wa jimbo la Arusha mjini,Mh. Godbless Lema kwa kosa la kuendesha mkutano wa hadhara bila kibali .

Aidha Jeshi hilo linawashikilia watu 67 wakiwemo wabunge wanne wa Chadema kwa kosa la kufanya mkusanyiko usiokuwa na kibali katika uwanja cha Soweto jijini hapa.
Akiongea na waandishi wa habari,Kamishna wa Polisi, Paul Chagonja Alisema kuwa wanawasaka wabunge hao baada ya kukimbia kusiko julikana mapema jana mara baada ya kufanya mkutano pasipo kuwa na kibali cha mmiliki wa kiwanja (AICC) pamoja na Jeshi la Polisi .

Aliwataja wabunge ambao wamekamatwa na jeshi hilo kuwa ni pamoja na mbunge wa singida,mh. Tundu Lissu ,Mbunge viti maalumu Joyce Nkya,mbunge wa Mbulu Mustafa Akunay pamoja na Saidi Arifu ambapo wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mapema kesho mara baada ya kupata Dhamana wakiwa katika kituo kikuu cha polisi mkoa.

Sanjari na hilo pia kamishna huyo alisema kuwa jeshi hilo linawataka viongozi hao wawili wa Chadema kuja kutoa ushahidi wa mlipuko wa bomu uliotokea Jun 15 katika kiwanja cha Soweto wakati mkutano wa chadema wa kufunga kampeni ulipokuwa unafanyika kwani viongozi hao walidai kuwa wanao ushaidi wa kutosha wa picha na video zinazoonyesha muhusika wa kitendo hicho cha ulipuaji .

“kama kweli Mbowe na Lema wanamapenzi mema na wakazi wa Arusha na uchungu wa damu ya wananchi iliyomwagika wajitokeze kulisaidia jeshi la polisi kutoa ushahidi huo ,ili muhusika aweze kufikishwa kwenye vyombo vya dola, kwani polisi sio wauaji bali wasimamia ulinzi na haki ya wananchi wake na kama basi wataona hawataki kutoa ushaidi kwetu na wanatuhisi vibaya kama wanavyo sema basi wapeleke ushaidi huo kwa Rais wa nchi maana yeye ndie Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchi”alisema Chagonja.

Aliongeza kuwa kama wataona pia huko hapafai kupeleka basi watafute shehe au padre wapeleke ushahidi huo na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtu huyo ambaye amehusika.

Aidha alibainisha kuwa endepo hawata fanya hivyo sheria itafata mkondo wake kama inavyosema kuwa iwapo mtu anaushaidi wa kosa la jinai na anakaa nao pasipo kuutoa kwa vyombo vya dola basi mtu Yule nae atachukuliwa hatua za kisheria ya yeye pia kufunguliwa mashtaka ya kosa la jinai.

Pia aliwataka wakazi wa mkoa wa Arusha kuendela na shughuli zao huku wakijiepusha na makundi ya kisiasa pamoja na mikusanyiko isiyokuwa na kibali kwani kufanya hivyo ni kuendeleza machafuko huku wahusika wakiwa wanatafuta mkono wao kwenda kinywani .

Aidha aliwataka waandishi wa habari kuwa wazalendo kwa nchi yao na kutumia kalamu pamoja na kamera zao kulinda na kutunza amani ya nchi ikiwemo kuheshimimu sheria kwa kuandika habari za kweli zenye kulinda amani kuliko kuleta machafuko.


Waziri mkuu Pinda azindua mradi wa kuimarisha halmashauri za miji 18 Tanzania bara

Waziri mkuu Mizengo Pinda akikata utepe katika vitabu kuashiria kuzinduliwa kwa mradi wa kuimarisha halmashauri za miji 18 Tanzania bara,Uzinduzi huo uliofanyika mjini Moshi.Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi, Hawa Ghasia na kulia ni Mwakilishi wa benki ya dunia,mkurugenzi mkazi Philippe Dongies wakishuhudia.
Waziri mkuu Mizengo Pinda akiwahutubia washiriki wa warsha ya uzinduzi wa mradi wa kuimarisha halmashauri za miji 18 Tanzania bara uliofanyika mjini Moshi.
Washiri wa warsha hiyo.


mapitio ya magazeti leo


Kili Music Tour 2013 kuanzia Dodoma jumamosi juni 22

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) chini ya Bia yake ya Kilimanjaro, inataraji kuanza rasmi tamasha kubwa la muziki lijulikanalo kama ‘Kili Music Tour’ wikiendi hii katika mji wa Dodoma.

Tamasha hii kubwa linatarajiwa kuanza siku ya Jumamosi ya tarehe 22 Juni, 2013 mjini Dodoma kwenye viwanja vya Jamhuri na litajumuisha wasaniii 8 ambao ni Ally Kiba, Ommy Dimpoz, Professor J, Ben Pol, Lady Jay Dee, Lynex, Roma na Kala Jeremiah.

Mwaka huu Bia ya Kilimanjaro imebadilisha utaratibu wa tamasha hili la muziki ambalo lilikuwa linajulikana kama KTMA Winners Tour na lilikuwa likijumuisha wasanii walioshinda tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards pekee.

Mwaka huu bia ya Kilimanjaro imebadilisha jina la tamasha kuwa Kili Music Tour na litashirikisha wasanii wote kwa ujumla na sio washindi wa tuzo za KTMA pekee.

“Kili Music Tour imepanua wigo wake kwa kushirikisha wasanii walioshinda tuzo, wasanii waliokuwa kwenye mapendekezo ya tuzo na wasanii ambao hawakushiriki kabisa kwenye tuzo lakini wako juu kwenye tasnia ya muziki nchini. 

Hii ni kwenye kuhakikisha kuwa mashabiki wa muziki wanapelekewa wasanii wanaowapenda kwenye mikoa yako bila kubagua. Mwaka huu matamasha yameongezeka kutoka sita mwaka jana na kuwa nane.

Kili inaelewa ni jinsi gani watanzania wanajivunia mambo ya kitanzania kama muziki wetu wa bongo flava, dansi yetu ya kiduku, kandanda letu lenye ushabiki wa simba na yanga, lugha yetu ya kipekee na bia yetu ya Kilimanjaro inayowapa bonge la kiburudisho .

Ndio maana tumeongeza wigo wa Tamasha kama ishara ya shukurani kwa jinsi watanzania wanavyojivunia mambo ya kikwetu kwetu.” Alisema Bwana George Kavishe Meneja wa bia ya Kilimanjaro.

Msanii aliyebobea wa bongo flava ajulikanaye kama Kala Jeremiah naye alisema “ mwaka huu mashabiki wategemee kupata vionjo ambavyo hawajawai kuviona kwani mimi na wasanii wenzangu tumejipanga kikamilifu kuhakikish kuwa hatuwaangushi mashabiki wetu na kuwa tunawapa bonge la kiburudisho!” 


Benki ya BADEA yaisaidia Serikali ya Tanzania katika miradi ya maji na kituo cha hesabu

Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa akiongea jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) Abdelaziz Khelef wakati wa utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa (kushoto) akimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) Abdelaziz Khelef mara baada ya kumalizika utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe akipongeza Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Kuli ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) Abdelaziz Khelef.
Baadhi ya maofisa kutoka Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) wakifuatilia utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.Picha na Anna Nkinda - Maelezo.


Mpigie Kura yao Mshiriki Nando ili aweze endelea kubaki ndani ya jumba la Big Brother


Furaha ya burudani ya miaka ilee sasa imerejea

Furaha ya burudani ya miaka ilee sasa imerejea. Melegendari sasa wamekiri kuwa walichokikosa kwa muda mrefu, sasa kinapatikana isumba lounge -jollies club kila ijumaa na j'mosi. Ni katika night of the legends na DJ John Dillinga aka The Legend is Back, DJ Fast Eddy na DJ Young Kelvin. Njoo ujumuike na malegendari wenzako ukumbukie wakati muziki ukiitwa muziki. Milango iko wazi saa 3 usiku, kiingilio 10,000/-. Karibu sana. 4 more info or comments like facebook page @www.facebook.com/pages/DJ-JD or follow instagram @DJJDTHELEGEND


RAIS KIKWETE AREJEA NCHINI BAADA YA ZIARA YA KIKAZI NCHINI UINGEREZA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza kwa makini maelezo aliyokuwa akipewa na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea nchini Uingereza. Rais Kikwete alirejea nchini tarehe 18.6.2013 usiku baada ya ziara ya kikazi nchini Uingereza. PICHA NA JOHN LUKUWI


New UNHCR report says global forced displacement at an 18-year high ;Tanzania hosting the 5 th largest refugee camp




SHUKRANI

Familia ya Bw. Thomas Martin Kiama, aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwa mara nyingine tena, kwa moyo mkunjufu tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ndugu, jamaa, marafiki, wafanyakazi wenzetu na wote wenye mapenzi mema kwa kutufariji kwa hali na mali wakati wa msiba wa mpendwa mama, dada, bibi, rafiki na mke Victoria Thomas Kiama uliotokea tarehe 11 Mei, 2013.

Kwa upendo, tunawaomba wote kujumuika nasi katika Misa ya Shukrani itakayofanyika Jumamosi tarehe 22 Juni, 2013 katika Kanisa Anglikana la Mt. Albano, lilipo karibu na Posta Mpya saa 2 asubuhi, na baadae katika chakula cha mchana nyumbani, Mtaa wa Bongoyo, Oysterbay karibu na Ubalozi wa Kenya.

Tunamuomba Mungu wa Mbinguni aipumzishe roho ya Mpendwa wetu katika amani ya milele.

Amina.


WAJUMBE WA ALAT RUVUMA WASHAURI KUWEPO KWA MIPANGO YA MUDA MREFU

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma akitoa maelezo kwa mkuuu wa Wilaya ya Songea juu ya kikao chao cha ALAT ambacho wamejiwekea utaratibu wa kukutana kila baada ya miezi mitatu kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa ilani ya CCM.
Toka kulia kwako ni Katibu wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Mohemed Maje, Makamu mwenyekiti wa ALAT ambaye pia ni Menyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Stevini Nana, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho na Naibu meya wa Manispaa ya Songea Wiloni Kapinga wakipitia kablasha la kikao cha ALAT.Picha na Demasho Blog.


MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA YANAYOENDELEA NCHINI GHANA

Afisa Tawala Mwandamizi wa Wizara ya Fedha Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali Bw. Merkion Ndofi akimkaribisha mwananchi wa Ghana katika banda la Wizara ya Fedha.
Bw. William Ghump amabaye ni Ofisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi wa Wizara ya Fedha na Mkurungezi wa Utawala na Utumishi Bw. Peter Mapigano wa Benki ya Posta Tanzania pamoja Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma wakipanga mkakati wa uelimishaji umma katika banda la Wizara ya fedha.
Waziri wa Utumishi wa Umma ,Ofisi ya Rais Bi. Celina Kombani na Katibu Mkuu Bw. George Yambesi walipotembelea banda la Wizara ya Fedha hapa nchini Ghana.
Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi Ingiahedi Mduma akifafanua jambo kwa Bw. Eugene Koranteng Henaku wa Umoja wa Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Serilkali za Mitaa Nchini Ghana.


Warembo wa Redd's Miss Tanga 2013 watembelea Mapango ya Amboni jijini humo

Washiriki wa shindano la Redd's Miss Tanga 2013 wakiwa katika mapango ya Amboni jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya kutangaza utalii uliopo katika mkoa wa Tanga.Shindano lao litafanyika katika uwanja wa Mkwakwani Mjini Tanga siku ya Ijumaa Juni 22,2013.
Warembo wakiendelea na safari yao ndani ya Mapango hayo.
Washiriki wa shindano la Redd's Miss Tanga 2013 wakiwa nje ya mapango ya Amboni jijini Tanga ambako walitembelea ikiwa ni sehemu ya kutangaza utalii uliopo katika mkoa wa Tanga.Shindano lao litafanyika katika uwanja wa Mkwakwani Mjini Tanga siku ya Ijumaa Juni 22,2013.


mama Kkikwete apongezwa kwa kuendeleza soka nchini

Na Anna Nkinda – Maelezo
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amepongezwa kwa jitihada zake za kuinua sekta ya michezo nchini   jambo ambalo limewafanya  vijana wengi kujipata ajira katika fani hiyo.
Pongezi hizo zimetolewa jana na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Lindi  (LIREFA) Francis Ndulane wakati wachezaji wa timu ya Kariakoo ya mkoa huo walipozitembelea ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)  zilizopo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Ndulane alisema kuwa mchango unaotolewa na  Mama Kikwete umewapa hari na kuwatia  moyo vijana wengi na hivyo kuweza kuendeleza sekta ya michezo mkoani humo.
Alisema kuwa hapa nchini vijana wengi wana vipaji mbalimbali, lakini hawana watu wa kuwaendeleza, hivyo alimshukuru kwa jitihada zake za kuwaendeleza katika sekta hiyo na hivi sasa  wanaamini  kuwa wataweza kujiajiri na kuweza kuzisaidia familia zao.
Kwa upande wake Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA aliwapongeza wachezaji hao kwa juhudi kubwa wanayoifanya katika soka hadi kufikia hatua ya kushiriki ligi ya taifa ya mabingwa wa mkoa ngazi ya taifa na kufikia hatua ya nane bora.
Naye Mwenyekiti wa timu hiyo Abdalah Livemba aliwashukuru Mama Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe kwa moyo walionao wa kuisaidia timu hiyo hadi kufikia  hapo ilipo.
Alimuomba kuwatafutia mdhamini ili aweze kuwasaidia  kubeba mzigo mkubwa wa kuitunza timu hiyo ambao unaelekea kuwalemea.
Mama Kikwete aliikabidhi timu hiyo zawadi za  viatu pea 29, jezi seti mbili ambazo ni 32, mipira mitatu, pampu moja  na  soksi  pea 16.
Timu ya Kariakoo inashiriki mashindano ya ligi ya mabingwa mkoa ngazi ya Taifa ambayo yalianza tarehe 12/6/2013 kwa kuzishirikisha  timu 28 kutoka nchi nzima wao wamebaki kati ya timu nane na leo wanapambana na Friends Rangers ya mkoa wa Dar es Salaam mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam.






Zantel yazindua huduma ya taarifa za kilimo kwenye simu za mikononi.


 Mkurugenzi wa mazao wa wizara ya kilimo, chakula na ushirika, Dkt.Mshindo Msolla akisisitiza jambo wakati wa kuzindua huduma ya Z-KILIMO
 Wafabyakazi wa Zantel wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa wizara ya kilimo.

Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel, kwa kushirikiana na wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na kampuni ya Sibesonke leo wamezindua huduma mpya ya kutoa taarifa kuhusu kilimo kupitia simu za mikononi.
Huduma hiyo mpya inayofahamika kama,Z-KILIMO,itawawezesha wakulima nchini Tanzania kupata taarifa za papo kwa pao na uhakika kuhusu njia za kuendesha kilimo cha kisasa kwenye simu zao za mikononi.
Kupitia huduma hii ya Z-KILIMO, wakulima nchini, hata wale walio vijijini wataweza kupata taarifa muhimu za namna ya kuendesha kilimo cha kisasa na hivyo kuongeza uzalishaji na kukuza sekta nzima ya  kilimo. Akizungumza kwenye uzinduzi wa huduma hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Rasirimali watu cha Zantel, Francis Kiaga, amesema kwa kupitia huduma hii wakulima nchini watapata fursa ya kipekee kupata taarifa kuhusu kilimo moja kwa moja kupitia simu zao.

“Kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu, na kinachangia sana kwenye kukuza na kuchangia uchumi wa nchi yetu, na huduma hii imekuja wakati muafaka katika kuendeleza juhudi hizo, lakini pia kuwapa wakulima umuhimu wa huduma ya simu katika namna wanayoihitaji zaidi’ alisema Kiaga.

Akielezea zaidi huduma hiyo Kiaga alisema itawasaidia zaidi wakulima katika kuokoa muda ambao zamani waliupoteza katika kupata taarifa kuhusu kilimo, na pia kuwaongezea uzalishaji wa mazao yao.
Huduma ya Z-KILIMO pia itawapa wakulima taarifa kuhusu maandilizi ya ardhi, aina za mbolea, aina za mazao, aina za mifugo, aina ya magonjwa yanayoshambulia mazao, upaliliaji, taarifa za usafiri, hali ya hewa pamoja na sehemu ya majadiliano baina ya wakulima.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kilimo wa wizara, Daktari Mshindo Msola, alielezea kufurahishwa kwake na huduma akisema itasaidia kufungua fursa zaidi kwa wakulima nchini. ‘Kupitia huduma hii, wakulima sasa wataweza kuboresha mbinu zao za kilimo katika hatua zote za kilimo na hivyo kuongeza uzalishaji’ alisema Dkt Msola.
Nao kampuni ya Sibesonke, ambao wameingia ushirikiano wa kiteknolojia na wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na wizara ya maenedeleo ya Mifugo na Uvuvi, ukiwa na lengo la uwafikia watanzania wakulima kuwapa taarifa muhimu za kilimo kwenye simu zao.

“Sibesonke ina furaha kwa kuwezesha watanzania kufaidika na teknolojia hii kupitia mtandao wa Zantel’ alisema Daktari Uwe Schwarz, Mkurugenzi Mkuu wa Sibesonke. “Kampuni ya Zantel imeonyesha dhamira ya dhati katika kuhakikisha teknoljia hii inawafaidisha watanzania wote kwa mtandao wake ulioenea nchi nzima’ alisiistiza Daktari Schwarz.

Wakulima wanaweza kujiunga na huduma hii kwa kubonyeza *149*50#, ambapo wataweza kupata maelekezo ya kutumia huduma hii.  


UMOJA WA WAMILIKI WA MALORI TANZANIA WALALAMIKIA KUPANDISHWA KWA BEI ZA BIMA

 Msemamaji wa Umoja wa wamiliki wa Malori Tanzania, Bwana Elias Lukumay akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na malalamiko ya kampuni yake kuhusiana na ongezeko la bima. Kulia kwake ni Makamu mwenyekiti wa TATOA, Bi Angellina Ngalula.
 Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Malori Tanzania, Bi Angellina Ngalula akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na malalamiko ya umoja wao ya kupanda kwa bei za bima kwa asilimia 400. Kushoto kwake ni msemaji wa TATOA, Bwana Elias Lukumay.
=========  ========  =======  =========
UMOJA WA WAMILIKI WA MALORI TANZANIA WALALAMIKIA KUPANDISHWA KWA BEI ZA BIMA

Umoja cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) umelalamikia ongezeko la bei za bima, ukisema hazijazingatia uhalisia wa soko, pamoja na kukosa uhalali kwa kuwa hazijashirikisha wadau wa sekta ya usafiri pamoja na jamii kwa ujumla.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, msemaji wa TATOA Bwana Elias Lukumay, alisema wanasikitishwa na mamlaka ya uthibiti wa bima Tanzania (TIRA) kuongeza malipo ya bima kwa asilimia 400 bila kutoa sababu za msingi lakini pia bila kushirikisha wadau.

‘Majaribio yetu ya kuzungumza na TIRA yameshindika baada ya TIRA kutojibu barua wala mawasiliano rasmi ya kukutana nao, tofauti na makubalino yetu ya kikao cha mwezi wa pili, kati yetu na wao ambapo tulikubaliana kuwa na kikao kabla ya mazungumzo baina ya wadau na umma juu ya swala hili’ alisema Lukumay.

Akielezea zaidi kuhusu malalamiko hayo, Lukumay alisema vigezo maalumu vya kupandisha bei hizo haviko bayana lakini pia ushindani wa biashara haukuzingatiwa. ‘TATOA inaamini kuna njia nyingi za kufata ili kupandisha bei, lakini kubwa zaidi ni kuacha soko lijiendeshe lenyewe, kwani tuko kwenye soko huria’ alisema Lukumay.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa TATOA, Bi Angellina Ngalula, alisema ongezeko hili la bei ni kubwa mno kwa mara moja na litapunguza ushindani wa makampuni ya usafirishaji ya ndani, lakini pia litaongeza bei za usafirishaji kwa kiwango kikubwa sana na hivyo kuumiza uchumi wa nchi na mwananchi wa kawaida ataathirika kwa bei za bidhaa kupanda.

‘Sababu za TIRA kupandisha bei sio za msingi, sababu kama udanganyifu na kuongezeka kwa kesi za bima pamoja na ajali za barabarani, sio sababu tosha za kupandisha bima kwani kufanya hivyo kutaongeza malalamiko zaidi, na pia kuwavunja moyo wateja waaminifu’ alisema Bi Ngalula.

Bi Angellina pia alitoa wito kwa wahusika, yaani TIRA, kuacha tamaa na kutokuendeshwa na genge la makampuni ya bima na kurudi kwenye meza ya majadiliano ili kuweza kupata muafaka kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi kwa maendeleo ya taifa.

‘Bila TIRA kurudi kwenye meza ya majadiliano TATOA itabidi ichukue hatua mbadala kama kwenda mahakamani na kugomea bei hizi mpya, jambo ambalo litasababisha usumbufu kwenye uchumi wetu’ alisitiza Bi Ngalula.


miondoko ya kumeremeta kwenye mnuso


mkataa kwao mtumwa


ngoma azipendazo ankal


Watanzania wa Nurnberg katika Afrika Festival Nurnberg,UJERUMANI

Watanzania waishio kwenye mji wa Nurnberg na sehemu za jirani na mji huo nchini Ujerumani,wameshiriki vyema Maonyesho ya Afrika Festival Nurnberg iliyofanyika kuanzia tarehe 13.-16. Juni 2013 mjini huo.Wageni mbali mbali walifanikiwa kutembelea Banda la Tanzania kujionea mambo mbali mbali yaliopo nchini kwetu.
Bwana Ramadhani Barungi akitoa maelezo kwa mgeni.
pilikapilika katika Banda la Tanzania.
Wageni wakionja maandazi na chapati.
Bwana Mukada Kidawa kushoto na Bwana Erick Morro, mwenyekiti wa Watanzania Nurnberg wakipokea msaada wa vifaa vya michezo na muziki kwa ajili ya Taasisi ya Talent Search and Empowerment.