Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.
KAMPUNI ya Tanzania Home Expo inatarajia kufanya maonyesho ya bidhaa zake  mbalimbali katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam,Mei 3o hadi Juni mosi mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Home Expo,Zenno Ngowi wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO leo jijini Dar es Salaam.

Ngowi  amesema kuwa katika maonyesho hayo ya  matano ,Wananchi wajitokeze  kwa wingi ili kujua nini wanafanya na pia ni namna gani mikopo ya nyumba inaweza kupatikana kwa urahisi na kwa gharama  nafuu, kwakuwa katika maonyesho hayo kutakuwa na watu wanaotoa elimu juu ya mikopo nafuu.

Ameongeza kuwa watatoa elimu na njia ya upatikanaji wa nishati mbadala,ujenzi nafuu na uendelezaji wa upatikanaji wa makazi bila gharama yeyote.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Home Expo,Zenno Ngowi akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya Habari MAELEZO leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na wananchi wajitokeze kwenye maonyesho ya 5 ya Tanzania Home Expo, ambapo kutaonyeshwa jinsi wanavyo fanya kazi na namna mbalimbali ambazo wanaweza kupata mikopo ya nyumba kwa bei rahisi kutoka kwenye mabenki mbalimbali hapa nchini, kushoto ni Afisa Masoko wa EAG Group Ltd Helen Mangare na Kulia ni Afisa Masoko wa EAG Group Ltd, Richard Raymond.
Baadhi ya waandishi wa habari walio hudhuria katika mkutano wa kuhamasisha wananchi kwenda kwenye maonyesho ya 5 ya Tanzania Home Expo yatakayofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam kuanzia ijumaa wiki hii. PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...