Mkuu
wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akizungumza na waendesha pikipiki
(Maarufu kama Boda Boda) leo hii katika ukumbi wa Songea Club uliopo
Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma. Mwambungu amewataka dereva Boda boda
kuepusha ajali za barabarani kwa kufuata sheria,kutotumiwa katika
maandamano ya kisiasa ambayo yanapelekea uvunjifu wa amani na kuwafanya
wapoteze maisha ama kuwafanya kuwa walemavu.
Pichani
ni umati wa waendesha pikipiki wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma
wakimsikiliza mkuu wa Mkoa ambaye hayupo pichani. Ambapo katika mkutano
huu amewaasa mambo mengi ikiwemo suala lililotokea hivi karibuni la
kuwarushia bomu askari polisi waliokuwa kwenye doria na kuwajeruhi
askari wa tatu.
Madereva
pikipiki hawa wakimsikiliza mkuu wa mkoa kwa umakini huku wakiahidi
kutoa ushirikiano wa kuwafichua wahalifu ambao wamejiingiza katika
huduma ya kusafirisha abiria kwa lengo la kuwachafua na wao kukidhi
mahitaji yao.
Piki piki zikiwa zimepaki nje ya mkutano.(Picha zote na demasho.com)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...