Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akizungumza na waendesha pikipiki (Maarufu kama  Boda Boda) leo hii katika ukumbi wa Songea Club uliopo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma. Mwambungu amewataka dereva Boda boda kuepusha ajali za barabarani kwa kufuata sheria,kutotumiwa katika maandamano ya kisiasa ambayo yanapelekea uvunjifu wa amani na kuwafanya wapoteze maisha ama kuwafanya kuwa walemavu.
 Pichani ni umati wa waendesha pikipiki wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wakimsikiliza mkuu wa Mkoa  ambaye hayupo pichani. Ambapo katika mkutano huu amewaasa mambo mengi ikiwemo suala lililotokea hivi karibuni la kuwarushia bomu askari polisi waliokuwa kwenye doria na kuwajeruhi askari wa tatu.
Madereva pikipiki hawa wakimsikiliza mkuu wa mkoa kwa umakini huku wakiahidi kutoa ushirikiano wa kuwafichua wahalifu ambao wamejiingiza katika huduma ya kusafirisha abiria kwa lengo la kuwachafua na wao kukidhi mahitaji yao.
Piki piki zikiwa zimepaki nje ya mkutano.(Picha zote na demasho.com)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...