Na. Catherine Sungura.
Wazazi nchini wametakiwa kuwakinga watoto wao wakati waendeshapo magari kwa kuhakikisha wanawafunga mikanda ili kuwaepusha na ajali za barabarani na kudhibiti madhara yatokanayo na ajali.

Rai hiyo imetolewa leo jijini hapa na kaimu  kamanda kikosi cha usalama barabarani Tanzania,Kamishna Msaidizi wa Polisi Fortunatus Musilimu    wakati akifungua  mafunzo kwa Mawakili,Mahakimu ,Waendesha Mashitaka na Askari wapelelezi wa kesi za ajali za barabarani,iliyoandaliwa na wizara ya afya kwa kushirikiana na shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia mpango wa Bloomberg Initiative Global Road Safety.

Alisema wazazi wengi wanapokuwa wanaendesha magari hawawafungi mikanda watoto wao na hivyo ajali inapotokea watoto wanakuwa ni wahanga wakubwa kwa kupoteza maisha au kupata ulemavu wa kudumu
“Wazazi mnawalindaje watoto,baba anaendesha gari,mtoto yupo kwenye usukani anaendesha nae gari,hiyo siyo sahihi ,tuwalinde watoto wawe salama kwa kuvaa mikanda”

Aidha, Kamanda   Musilimu alisema tatizo la ajali barabarani nchini imekua ikiongezeka kila mwaka na hii ni kutokana na wananchi kutokuona kama ajali ni tatizo kubwa na la haraka ambalo linafanya kuongezeka kwa vifo nchini kulinganisha na magonjwa mengine na hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa kiuchumi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...