Na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amewapongeza wabunge kwa kushiriki vizuri mashindano ya Muungano yaliyofanyika Zanzibar na kurudi salama mjini Dodoma kuendelea na majukumu yao.

Pongezi hizo za Spika zimetolewa leo Bungeni Dodoma na Naibu Spika Dkt. Tulia Akson kwa niaba ya Spika alipokuwa akitoa matangazo kabla ha kuahirisha shughuli za Bunge hadi jioni ambapo Bunge linaendelea kujadili hoja ya Hotuba za Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora inayoongozwa na Mawaziri George Simbachakene na Angella Kairuki iliyowasilishwa mapema leo.

Timu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizoshiriki mashindano hayo ni timu za mpira wa miguu na pete ambapo timu ya mpira wa pete imefanya vizuri kwa kuishinda timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwa magoli 18 kwa magoli 15 wakati timu ya mpira wa miguu zilitoka sare ya kufungana goli 1:1 Kushiriki kwa Wabunge katika mashindano hayo yamelenga kuimarisha udugu uliopo kati ya pande mbili za Muungano na kuwapa fursa Wabunge kufanya mazoezi kwa ajili ya kujenga na kuimarisha afya zao.

Aidha, michezo kwa Wabunge inatoa nafasi kubwa ya ushirikiano ambayo ni kielelezo cha msingi kinachozaa Viongozi bora wanaotokana na sekta ya michezo. Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wanafursa kubwa ya kufanya mazoezi mbalimbali katika kujenga na kuimarisha timu za Bunge hilo ili kujenga pia ujirani mwema.

Ushiriki wa Wabunge kwenye mashindano siyo mara ya kwanza, Wabunge hao hushiriki michezo mbalimbali, wanashiriki mpira wa miguu wakiwa watani wa Jadi wa timu za Simba na Yanga, Februari 4, 2012 walishiriki mazoezi ya viungo yaliyoendeshwa na klabu inayojulikana kama “Kitambi noma” kutoka mjini Unguja kwa kuzingatia Bunge lina eneo mahususi la kufanyia mazoezi mazoezi ya viungo (Gym).
Naibu Spika Mhe. Dkt. Tulia Akson akitoa maelekezo wakati wa mkutano wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalum Tabora mjini Mhe. Mwanne Nchemba (CCM) akichangia hoja wakati kujadili hoja ya Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora inayoongozwa na Mawaziri George Simbachakene na Angella Kairuki iliyowasilishwa mapema leo Bungeni mjini Dodoma.
Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema (CHADEMA) akichangia hoja wakati kujadili hoja ya Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora inayoongozwa na Mawaziri George Simbachakene na Angella Kairuki iliyowasilishwa mapema leo Bungeni mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...