SHIRIKA la kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) limeeleza kuwa waandishi wa habari takriban 700 wameuawa katika kipindi cha miaka 10, huku zikionyesha wastani kuwa kila baada ya wiki moja mwandishi mmoja anauawa duniani.

Pia ilisema kwa mujibu wa ripoti ya waandishi wasio na mipaka kuhusu matukio ya uhuru wa waandishi wa habari, Tanzania imeshuka kwa nafasi sita ambapo hapo nyuma ilikuwa nafasi ya 69 kati ya nchi 180 kati ya mwaka 2006 mpaka 2014, lakini kwa mwaka 2015 ipo katika nafasi ya 75.

Akizungumza katika mkutano uliowajumuisha wataalamu wa habari, jijini Dar es salaam, Mwakilishi Mkazi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues, alisema asilimia 94 ya waandishi hao ni wale wa ndani ya nchi na kwa vyombo vya habari vikubwa ambapo chache kwa waandishi wa kigeni.

Alisema kutokana na matukio hayo, ilichochea kwa UNESCO kufatilia na kujua tatizo kubwa na kuandaa agenda chini ya Umoja wa Mataifa(UN) ili waandishi waweze kuwekewa usalama katika maeneo yao ya kazi.

“UNESCO tulilaani vitendo hivi na tuliweza kusikiliza kesi takribani 540 za waandishi, pamoja na kutafuta chanzo cha tatizo hili na njia ya kuweza kuliondoa,” alisema Zulmira.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza na wandishi wa habari (hawapo chani) juu ya waandishi wa habari takriban 700 waliouawa katika kipindi cha miaka 10, huku zikionyesha wastani kuwa kila baada ya wiki moja mwandishi mmoja anauawa duniani, katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel, akifafanua jambo katika mkutano huu ulio fanyika leo jijini Dar es Salam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel,akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa habari walio fika katika mkutano huo ulio fanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...