Mahmoud Ahmad Arusha
WATANZANIA 500,000 wanatarajiwa kutembelea mbuga zote 16 za hifadhi za taifa mwaka huu ikiwa ni hatua ya kuimarisha na kukuza utalii wa ndani ambapo watajionea vivutio mbalimbali vilivyomo ndani ya hifadhi hizo.

Hayo yameelezwa leo na Meneja uhusiano wa shirika la hifadhi za taifa, Tanapa, (Pichani)Pascol Shelutete, makao makuu ya TANAPA, jijini ,Arusha,  alipokuwa akizindua hatua ya mwisho ya  kampeni  maalumu ya miezi sita ya  kuhamasisha Watanzania kutembelea hifadhi  ili kujionea vivutio kwenye hifadhi wanazopakana nazo ili kuimarisha utalii wa ndani 

Kampeni hiyo ni Makakati maalumu uliobuniwa na Tanapa,  unaotoa  hamasa kwa watanzania kutembelea mbuga za hifadhi zilizopo karibu na maeneo yao kwa gharama nafuu hasa siku za mwishoni mwa wiki na hivyo kuwapunguzia matumizi ya fedha wanazotumia kwenye starehe na badala yake wazitumie kutembelea hifadhi .

Meneja uhusiano wa Tanapa,  Shelutete, amesema kuwa  kadiri miaka inavyozidi kusonga mbele mwamko wa watanzania kutembelea mbuga za hifadhi unaongezeka, ambapo mwaka 2013 watanzania 362,217, walitembelea hifadhi zote 16 nchini, na mwaka 2014 watanzania 427,258 wametembelea mbuga hizo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...