Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipokea Rufaa za Wabunge 55 na imeshatolea maamuzi rufaa 42 bado rufaa za Wabunge 13
ambazo vielelezo vyake vinasubiriwa kutoka kwenye Halmashauri husika.
Kulikuwa
na Rufaa 16 za Wabunge waliokuwa wameenguliwa. Kati ya hizo Wabunge 13 wamerudishwa kuendelea na
kampeni na rufaa 3 Tume ilikubaliana
na maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi hivyo hao hawatarudishwa kwenye orodha ya
Wagombea.
Aidha, rufaa 24
zimekataliwa na Tume ambapo maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi yataendelea
kubaki kama yalivyo na wagombea wataendelea kugombea. Pia kuna rufaa 2 ambazo Tume haijazijadili kwa
kuwa hazikufuata utaratibu wa kuwasilisha Tume yaani kupitia kwa Wasimamizi wa
Uchaguzi wa Majimbo husika hivyo, maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi yatabaki
kama yalivyo na wagombea wataendelea kugombea kama walivyoteuliwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...