RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ( Pichani)amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imeandaa mipango na sera nzuri za kuwasaidia vijana ili waweze kujiajiri
wenyewe hasa waliojiunga katika vikundi vya ushirika na SACCOS.
Dk. Shein alisema
kuwa Serikali imeanzisha Mfuko wa kuwawezesha Wananchi Kiuchumi na tayari watu
kadhaa wameanza kufaidika na Mfuko huo sambamba na kuwapatia mafunzo ya
kitaalamu pamoja na kuvipatia vikundi vya ushirika mbinu za kupata masoko na
kuwawezesha kuwa wajasiriamali wazuri.
Akisoma hotuba
kwa niaba ya Dk. Shein Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara
Maalum, Mhe. Haji Omar Kheir, aliyasema hayo leo katika uzinduzi wa Jumuiya ya
Watazania Wasio na Ajira (TUEPO) huko katika ukumbi wa afisi za Jumuiya hiyo
Rahaleo, mjini Zanzibar.
Aidha, Dk. Shein
alisema kuwa katika kuwasaidia vijana walioshindwa kuendelea na masomo yao,
Serikali imeyaimarisha mafunzo ya elimu ya amali katika vituo vya amali vya
Mwanakwerekwe na Mkokotoni Unguja na Vitongozi huko Pemba.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...