Na  Bashir  Yakub.

Mara  kadhaa kwenye  familia  mbalimbali   kumekuwa hakuna  maelewano  juu  ya  nani  asimamie  mirathi. Unakuta  wapo  wanaomkubali  fulani  asimamie  na  wapo  wanomkataa  wakimtaka   fulani  mwingine  ndiye  asimamie.  Hii   huwa  na  athari  kubwa sana  kwa  warithi  hasa  watoto  kama  wanasoma  ambao  kimsingi  hutakiwa kutumia mali  zile katika  mahitaji  ya  msingi  kama  ada  na  mahitaji  mengine muhimu ya  kiustawi. 

Tumeshashuhudia  mara  nyingi  watoto  wakiacha  kwenda  shule  kwa  kukosa ada  na  mahitaji  mengine  muhimu  kwa  ustawi  wao sababu  kubwa  ikiwa  mgogoro  wa  nani  awe  msimamizi  mirathi. Naamini  huwa hakuna sababu  za  msingi  za kufikia   huko kwakuwa  tayari  sheria imetoa  mwongozo  wa  nini  kifanyike  katika  mazingira kama  hayo.  Utata  huu  mara  nyingi  husababishwa  na  kutokuaminiana  hasa  kama  ndugu  wana  utofauti  wa  mmoja wa wazazi  mama  au  baba. Makala  yataeleza lipi  la  kufanya.

1.MAMBO  YANAYOZINGATIWA  NA  MAHAKAMA  KUTEUA MSIMAMIZI  MIRATHI.
( a ) Kwanza  mahakama  huangalia  kama kuna  wosia.  Iwapo  kuna  wosia  basi  huangalia  iwapo  wosia  ule  umemtaja  msimamizi  wa  mirathi. Ikiwa  umemtaja   msimamizi  wa  mirathi    na  hakuna  shauri  lolote  lililofunguliwa kupinga  au  kuhoji  uhalali  wa  wosia  huo   basi  msimamizi  wa  mirathi  aliyetajwa  ndani  ya  wosia  huo ndiye  atakayethibitishwa  rasmi na  mahakama    kama  msimamizi  halali  wa  mirathi.

( b ) Uadilifu  wa  mwombaji  ni  jambo  jingine  muhimu  linalozingatiwa  sana  na mahakama   kabla  kumteua  msimamizi  wa  mirathi. Yawezekana  mtu  akawa   ni  ndugu  wa  karibu  na  wa  pekee  wa  marehemu   aliyebaki    lakini  si  mtu  muadilifu. Ni mtu  ambaye  kukabidhiwa  amana  kubwa  ya  mirathi  ambayo  hukusanya  magari ,majumba  , mashamba   viwanja  n.k  itakuwa ni  sawa  na  kuzitupa  mali  hizo.  

Lakini  pia  uadilifu  asiwe  ni  mtu  ambaye   ana  upendeleo  kiasi  akikabidhiwa  mirathi hawezi  kutenda  haki   baina  ya  warithi.  Watu  wenye  sifa  hizo  hawatateuliwa  kusimamia  mirathi. Hata  hivyo hayo  yatatakiwa kuibuliwa  na  kuoneshwa  na  wanaompinga  msimamizi  aliyependekezwa  kwa kupeleka  pingamizi  mahakamani. 

( c )  Jingine  linaloangaliwa  ni  maslahi  ya  muombaji  kwa  marehemu  au  kwa  mali  za  marehemu.  Maslahi  kwa  marehemu huangaliwa  ukaribu  wa  udugu  kwa  mfano  huyu ni  mjomba  wa  marehemu  na huyu  ni  mtoto  wa  marehemu. Kimsingi  mtoto  wa  marehemu atakuwa  na  nafasi  kubwa  ya  kuwa  msimamizi  wa  mirathi kuliko  mjomba  wa  marehemu.  Aidha maslahi  kwa  mali  za  marehemu  huhusisha  wadeni  wanaomdai  marehemu  kwa  mfano  mabenki n.k. Hawa  nao  wanaweza  kuomba na  kukubaliwa  kuwa  wasimamizi  wa  mirathi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...