THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa masikitiko na huzuni nyingi taarifa ya kifo cha mwanasiasa mkongwe nchini na aliyepigania uhuru wa Tanganyika, Ndugu Samwel Ntambala Ruangisa, ambaye aliaga dunia mwanzoni mwa wiki hii nchini Marekani ambako alikuwa anatibiwa.

Katika salamu za rambirambi ambazo amempelekea Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mheshimiwa John Mongella kuomboleza kifo cha Mzee Ruangisa, ambaye pia alikuwa bado diwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Rais Kikwete amesema:

“Nimepokea taarifa za kifo cha Mzee Ruangisa kwa masikitiko na huzuni nyingi. Kwa zaidi ya nusu karne, Mzee Ruangisa amekuwa kiongozi wa kuigwa mfano katika nafasi zote ambazo zimepata kuzishikilia katika maisha yake kuanzia Ukuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi (sasa Kagera) na baadaye Mkoa wa Mara tu baada ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Ubalozi, Uwaziri, Ubunge, Umeya na Udiwani. Katika kila nafasi aliyoishikilia, Mzee Ruangisa alionyesha uongozi wa kiwango cha juu. Kwa hakika, tumepoteza kisima cha uzoefu wa uongozi.”

Rais Kikwete ameongeza katika salamu zake za rambirambi: “Mkuu wa Mkoa nakutumia salamu zangu za rambirambi kuomboleza msiba huu na kupitia kwako naomba uwape pole wana-Kagera wote kwa kuondokewa na mzee wao wa siku nyingi. 

Aidha, naomba unifikishe pole zangu nyingi kwa wanafamilia wote ambao wamepoteza baba, babu na mhimili wa familia. Wajulishe kuwa niko nao katika kipindi hiki kigumu. Waambie naelewa machungu yao kwa sababu machungu yao ni machungu yangu. Vile vile, naungana nao katika kumwomba Mwenyeji Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweke peponi roho ya Marehemu Samwel Ntambala Ruangisa. Amina.”

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU,
DAR ES SALAAM.

27 Mei, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...