Mkurugenzi Mkuu  wa TFDA , Bw. Hiiti B. Sillo akitoa hotuba ya TFDA kukubali kujiunga na Umoja wa Nchi za Asia katika Udhibiti wa Vifaa Tiba na Vitendanishi (Asian Harmonization Working Party on medical devices and diagnostics - AHWP) wakati wa mkutano wa mwaka wa AHWP uliofanyika Seoul, Korea Kusini kuanzia tarehe 17 - 21 Novemba 2014. Tanzania imekubaliwa rasmi kuwa mwanachama 24 wa AHWP  ikiwa  ni  nchi  ya pili Barani Afrika kujiunga  na  umoja huo baada  ya Afrika Kusini.
 Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti B. Sillo akiwa na Mwenyekiti wa umoja huo Dkt. Saleh Al –Tayyar  kutoka Saudi Arabia baada ya kukabidhiwa mwongozo rasmi TFDA wa kuimarisha mfumo wa udhibiti wa vifaa tiba na vitendanishi kama mwanachama mpya wa umoja huo.

Mwenyekiti  wa AHWP , Dkt. Saleh Al –Tayyar  kutoka Saudi Arabia akiwapongeza Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti B. Sillo na Meneja wa Udhibiti wa Vifaa Tiba, TFDA, Bi. Agnes Sitta Kijo, baada ya Tanzania kujiunga rasmi kuwa mjumbe wa Umoja wa Wadhibiti wa Vifaa Tiba katika nchi za Asia (AHWP).
 Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti B. Sillo akisalimiana  na Waziri  anayesimamia Usalama wa Chakula na Dawa nchini Korea na kati yao ni Mwenyekiti wa AHWP  Dkt. Saleh Al –Tayyar .





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...