Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Diamond
Trust Bank (DTB), Bw. Abdul Samji, akisaidiana kukata utepe na Meya wa Jiji la
Mtwara, Mhe. Seleman Mtalika, wakati wakizindua tawi jipya la benki hio jijini
Mtwara. DTB kwa sasa ina matawi 21 nchi nzima, na inapanga kufungua matawi
mengine manne (4) kwaka 2015, kuongeza nguvu kwa mtandao wake kwa miji ya
Mwanza na Dar es Salaam.
======== ======= =======
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Diamond
Trust Bank Tanzania Limited (DTBT), Abdul Samji, amezindua tawi la Benki hiyo
katika Manispaa ya Mtwara, lililopo katika Barabara ya Tanu, na hivyo kufanya
Benki hiyo kuwa na matawi 21 nchini Tanzania.
Wakati Mwenyekiti Abdul Samji akizindua
tawi la kwanza la DTB kwa Mikoa ya Kusini, alionyesha furaha yake kwamba kwa
kipindi cha miaka 7 Diamond Trust Bank imefungua matawi mapya yapatayo 17 –
wastani wa matawi 2 hadi 3 kwa mwaka. “Benki yetu ilianza na matawi 4 mwaka
2007 na leo ina matawi 21, huku tukiwa na mpango wa kufungua matawi mengine
mawili ndani ya miezi mitatu ijayo,” alisema Samji huku akionesha uso wa
furaha.
Akizungumza na wanahabari wakati wa
sherehe za uzinduzi rasmi wa tawi hilo, Samji amesema Benki yake imejizatiti na
mpango wake wa kuendelea kufungua matawi nchini. “Kufunguliwa kwa Tawi la DTB
katika Manispaa ya Mtwara ni utekelezaji wa hamu na shauku iliyo nayo benki
yatu kuwa sehemu ya ukuzaji uchumi kwa mikoa ya kusini. DTB imekuwa ikitoa misaada
ya kibenki kusaidia miradi kadhaa ya maendeleo na ya kimiundombinu ili
kuwezesha kampuni zinazoendesha shughuli zao mkoani Mtwara. Tunaamini kuwapo
kwa DTB Bank kwenye mkoa huu kutawarahisishia mambo mengi wateja wengi wapya
watakaoanza kufanya nasi shughuli za kibenki.”
Sasa DTB inakuwa benki ya nane (8) ya
kibiashara kufungua tawi katika Manispaa ya Mtwara huku ikitoa huduma
kikamilifu za kibenki kwa wananchi wa Mtwara, na wakati huo huo ikiwa na
mikakati ya kuelekeza nguvu zake kwa wafanyabiashara ndogondogo na
wajasiriamali. Samji amesema kwamba DTB imejizatiti katika kuunga mkono
biashara ndogondogo ili kuziwezesha kupata haraka mikopo itakayowafaa.
Akizungumzia mpango wao wa kuungana na
Taasisi ya Aga Khan (Aga Khan Foundation-AKF) kuboresha mipango ya uchumi na
fedha, kilimo, uboreshaji wa maisha ya wananchi, elimu na afya Kusini mwa
Tanzania (kwenye Mikoa ya Mtwara na Lindi), Samji anasema: “Tumekuja Mtwara
tukiwa na uhakika wa kazi nzuri iliyofanywa na Taasisi ya Aga Khan (AFK)
miongoni mwa familia za wakulima wadogo wadogo katika Mikoa ya Kusini tukiwa
tumejizatiti kuunga mkono juhudi zao hizo za pamoja. Tunatarajia kwamba
kufunguliwa kwa Tawi la DTB la Mtwara, kutakuwa kama changamoto kwa programu ya
maendeleo ya Taasisi ya Aga Khan ambayo imedhamiria kuboresha maisha ya
wananchi wengi waishio vijijini katika eneo hili.”
DTB inachukuliwa kuwa ni Benki inayokua
kwa kasi kubwa sana nchini Tanzania; ikiwa na utendaji wa kiwango cha hali ya
juu sana katika tasnia ya viwango vya kibenki. DTBT imeripotiwa kuwa na kiwango
cha juu sana cha utendaji hadi kufikia mwishoni mwa Septemba 30, 2014 ikiwa
nyota katika ukuaji wa Faida Kabla ya Kukatwa Kodi (Profit Before Tax-PBT) ya
37.5% ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013. Faida kabla ya kodi
ilifikia kiwango cha TZS 15.4 bilioni hadi robo ya tatu mwaka 2014 ikiwa na
maongezeko ya kuvutia kutoka ukopeshaji na shughuli za fungani (treasury
activities).
Mali za Benki zimeongezeka kwa TZS 128
bilioni kutoka TZS 505 bilioni mwezi Desemba 2013 hadi kufikia TZS 633 bilioni
mwishoni mwa Septemba 2014, wakati mikopo kwa wateja (Net Advances to
Customers) imeongezeka kwa TZS 62 bilioni.
DTB kwa sasa ina matawi 21 nchi nzima,
matawi 8 yakiwa katika jiji la Dar es Salaam; mawili (2) jijini Arusha na tawi
moja moja katika miji ya Zanzibar, Tanga, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Moshi,
Morogoro, Iringa, Tabora, Kahama na ongezeko la tawi jipya la Mtwara. Benki
inapanga kufungua matawi mengine manne (4) mwaka 2015, kuongeza nguvu kwa
mtandao wake kwa miji ya Mwanza na Dar es Salaam huku kukiwa na uwezekano wa
kupata matawi mapya kwa miji ya Singida na Kigoma katika mwambao wa Ziwa
Tanganyika. Benki inaangalia kwa karibu uwezekano wa kupanua mtandao wake maeneo
ya Kusini mwa Tanzania katika miji ya Masasi, Lindi na Songea.
DTB Tanzania ni kampuni tanzu ya
makampuni ya DTB (DTB Group) kiuhusiano na East African Bank, na kufanya
shughuli za kibenki kibiashara na Kenya, Uganda na Burundi ikiwa na mtandao wa
matawi 107 kwenye ukanda huu.
DTB ni kampuni tanzu ya Mfuko wa Aga
Khan wa Maendeleo ya Kiuchumi (the Aga Khan Fund for Economic
Development-AKFED), ambayo ni tawi la Mtandao wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Aga
Khan (Aga Khan Development Network-AKDN).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...