Halmashauri zote Nchini zimetakiwa kuendelea kuhamasisha na kutoa Elimu kwa Wananchi juu ya
utunzaji wa mazingira na pia kuimarisha miundombinu ya masoko ambayo ni mibovu na ya kizamani.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu
wakati alipofanya ziara ya kutembelea masoko ya manispaa za Temeke na Ilala za jijini Dar es Salaam.
Amekumbushia pia kila Manispaa kuzingatia agizo la Makamu wa Rais la kufanya usafi kila jumamosi
ya mwanzo wa mwezi pia ametoa wito watu kutooneana aibu katika kutupa taka hovyo. Kila mtu awe
mlinzi wa mwenzie kuhakikisha anatunza mazingira ianavyotakiwa na pia hatupi taka hovyo, alisema
Mheshimiwa Ummy.
Katika ziara hiyo aliongea na wafanyabiashara katika masoko hayo na walimwambia changamoto
wanazokutana nazo katika swala zima la kudumisha usafi katika sehemu zao za biashara ni uhaba wa
maji na vifaa vya kufanyia usafi.
Ziara hiyo ni muendelezo wa ziara za mbalimbali za Viongozi wa Ofisi ya Makamu wa Rais katika
kuhakikisha utunzaji wa Mazingira unafanikiwa kwa kiasi kikubwa katika jiji la Dar es Salaam na Nchi ya
Tanzania kwa ujumla.
Naibu Wazir Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu akipata maelezo kutoka kwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Injinia Mussa Natty.
Naibu Wazir Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu akipata maelezo juu ya usafi wa
mazingira eneo la soko unavyofanyika. Anayetoa maelezo ni Mwenyekiti wa Soko la Tandale Sultan Ally
Kinombo.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu (katikati) akiwa katika ziara
kukagua soko la Temeke la Stereo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Temeke Protidas
Kagimbo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...