Mtakwimu, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Bw. Vilerian Kidole akifafanua juu ya
Umuhimu wa Tathmini ya Hali ya Chakula na Lishe Nchini kwa Wataalam kutoka kata
za Hedaru, Makanya na Vunta wakati wa mafunzo yanayoendelea Hedaru, Wilayani
Same juu ya jinsi ya kutekeleza Mradi Wa Kuijengea Jamii Uwezo wa kupunguza Athari
Za Maafa katika kata zao.
Mkuu wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Jamii, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania
Bi. Hellen Msemo akisisitiza juu ya Umuhimu wa Kutumia Taarifa za Mamla ya Hai ya
Hewa nchini katika Kupunguza Athari za Maafa kwa Wataalam wa kata za Hedaru,
Makanya na Vunta (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Tarehe
25 Agosti, 2014, Hedaru, Wilayani Same (katikati) katika mafunzo yanayoendelea
Hedaru, Wilayani Same juu ya jinsi ya kutekeleza Mradi Wa Kuijengea Jamii Uwezo wa
kupunguza Athari Za Maafa katika kata zao.
Mratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Jane Alfred akieleza jinsi jamii inavyoweza kukabili Maafa kwa Wataalam wa kata za Hedaru, Makanya na Vunta (hawapo pichani) katika mafunzo yanayoendelea Hedaru, Wilayani Same juu ya jinsi ya kutekeleza Mradi Wa Kuijengea Jamii Uwezo wa kupunguza Athari Za Maafa katika kata zao.
Baadhi ya Wataalam katika Sekta ya Kilimo, Mifugo, Afya, Elimu na Utawala wa kata
ya Hedaru, Makanya na Vunta wakinukuu masuala muhimu katika mafunzo hayo
yanayoendelea Hedaru, Wilayani Same juu ya jinsi ya kutekeleza Mradi Wa Kuijengea
Jamii Uwezo wa kupunguza Athari Za Maafa katika kata zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...